By Elikado Mwasenga
➡ Fuatana nami katika kujifunza neno la Mungu lanye uzimA
➡ Ntaka nkuletee mwendelezo wa somo tulilokuwa nalo
➡ ```Nlikupa sababu ya kwanza inayolenga mfumo wa taarifa unazozipa nafasi ndani mwako```
Na tukaona ya kuwa kwa kiwango kikubwa Sana vitu unavyovipa nafasi kusikilza kutazama nk nk maadam tu vna uhusiano na kuingiza taarfa ndan yako na kutengeneza mfumo wa kimaamuz(Fikra)
Vina uwezo wa either kukupa hatua Bora zaid au kukurudsha nyuma
Leo nakupa sababu ingine inaweza kuwa sababu ya ugumu unapitia watu wengine wanaita jarbu
Nataka tusome maandiko kidgo
📖 Warumi:3.23
kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;
Warumi:3.24
wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu;
Warumi:3.25
ambaye Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho
Yatazame kwa Makin maandiko haya
Anasema dhambi ilipoingia kwenye mfumo wa maisha ya mtu kilichofuata na *kuondolewa kwa utukufu wa Mungu juu yao*
Maana yake nn utendaji kaz wa Roho wa Mungu haupo juu yao tena
Na maandiko yako waz ya kwamba alipo Roho wa Mungu ndipo penye uhuru
Anhaa maana yake ni kwamba kuondolewa kwa utukufu(mazngra sahh kwa Roho wa Mungu kutenda kaz ndan na juu yako/yangu) kunaondoa na Uhuru
Na kuondoka kwa Uhuru kunazaa kitu kingine kinachoitwa jaribu/teso/gumu unaloanza kulipitia
Ukisoma msatari wa mbele kidgo utaona kwa huruma zake Mungu akaondoa hilo teso kwa neema yake kwa kunuweka Yesu awe upatanisho wa sisi na Mungu yaani kuurejesha utukufu wake
Swali langu linakuja kwako kwanini pamoja na kwamba tumehesabiwa haki kwa neema still tunakuna na magumu kwenye maisha yetu,,,,
Naomba uelewe vzur juu ya hili eneo anapozungumzia kuhesabiwa haki kwa neema
📖 Fungua namimi kitabu cha mathayo 6
Matayo:6.12
Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.
Matayo:6.13
Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.]
Matayo:6.14
Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi.
Ukisoma kwa makini maandiko haya na kutazama kile alichokisema kwenye warumi unaweza usielewe kidgo
Ngoja nkupe ufunuo wa ajabu kidgo
Kwanini nianze kuhangaika kuomba tena msamaha kwa Mungu na huku ninajua nimehesabiwa haki kwa neema
Yaaani kila kosa limefutwa kila laana haipo tena sasa kwanini niombe tena msaha??
➡ Kwanini
Mfano wewe mwanafunzi siku mkuu wako wa shule alipotangaza kila atakayepata " A" ya hisabati(mathematics) atampa zawadi alianza tu kugawa zawadi hata hamjaanza kufanya mtihani au alisubr mfanye mtihani aone matokeo ndipo agawe zawadi Sambamba na matokeo??
➡ Jibu unalo bila shaka
Pamoja na kwamba umeokoka umempa Yesu maisha yako hilo n Jambo moja kuna hatua ya ziada inahitajika
sijui kama unanielewa nnachotaka ukione hapa
haki tuliyohesabiwa hapa si kwamba haituhitaji tuombe toba mbele za Mungu hapana
Ni haki inayotupa uwezo wa kupokea msamaha kwa neema yaani tunasamehewa juu ya makosa tunayotubia japo kikawaida yalikuwa n makosa ambayo hata tungeomba msamaha tusingepata kusamehewa
➡ Hallelujah!
Kwa maana hiyo basi kuna watu tumo ndan ya yesu ila bado hatujajipatanisha naye kwa kiwango cha Yale magumu tunayokutana nayo kuondolewa
Sikia
Anasema hivi basi msali hivi,,,,
➡ Mstari wa13 anasema usitutie majarbuni(kwenye magumu)
➡Tafakari kwa kina hapa
Unataka kuniambia Mungu hajui kama sisi tumo ndan yake tunamuamini kwanini tena tumuombe atuepushe na majaribu na huku anajua hatutaki kujaribiwa??
Na kwa bahati mbaya Sana waamini wengi hawana tabia ya kuomba ombi hili la Mungu kuwaepusha na majaribu matokeo yake n kwamba wanajikuta wanajarbiwa na kuajarbiwa
Maisha yao ni Vita Vita magumu kila leo
Ukirsto wa namna hiyo mimi sioni raha yake hata kidgo
Mungu anataka tuEnjoy kuwa nayeye
Kwa hiyo sababu ingine inayopelekea kupitia ugumu unapitia n kwa sababu unakomaa Sana na hali yako
Wala sio mpango wa Mungu eti ukomae na hali yako kabisa sio mpango wa Mungu
Unasema kwa sababu gani unasema hivyo
Fungua na Mimi maandiko haya!
📖 Matayo:11.28
Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha .
Anataka umpe yeye masumbuko(magumu) yako mizigo yako ili upate pumnziko
Unajikuta unaanguka mara kwa mara kwenye zinaa
Unashia tu kusema leo ndo ilikuwa mwisho unajuta kabisa lakin siku mbili mingi usharud pale pale tena
Usipambane kwa nguvu zako nakwambia hutachomoka
Unapanga biashara yako unatafuta mtaji ukiaanza tu biashara hiyo haiana soko tena
Wala mbinu 12 za kuwa tajir ulizoziona YouTube hazitosh kukutoa hapo kuna nguvu ya ziada ya kiroho unahitaji
Kwa Nini umtwike yeye masumbuko na mizigo yako jibu hili hapa
📖 1 Petro:5.7
```huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.```
No comments:
Post a Comment