Part 1⃣
Elikado Mwasenga
Somo lenye kichwa umejiandaaje siku ile ijayo/ Are you prepared?
Kujiandaa kwa ajili ya mwisho wa miisho yote tuanze kwa kutazama maneno haya kutoka kwenye maandiko matakatifu,,,
π1 Petro:4.7
Lakini *mwisho wa mambo yote umekaribia* ; basi, *iweni na akili , mkeshe katika sala.
✝ Naomba usome kwa utulivu maneno haya
✝ NLT Bible. 1 Peter 4:7
[7] The end of the world is coming soon. Therefore, be earnest and disciplined in your prayers.
π 1 Peter 4:7 But the end of all things is at hand : be ye therefore sober, and watchful unto prayer
Kumbuka Jambo moja maneno haya yaliandikwa miaka zaid ya efu1 na miatano ilyopita
Lakini wale walioyaandika walikuwa serious nayo kuliko watu wa kizaz hiki tulichonacho
Tutatembea Sana na kifungu hiki Roho Mtakatifu atakupa ufunuo na Siri zilizopo kwenye hiki kifungu za kukujenga
Nianze tu kwa kusema kwamba kila Jambo huwa linakuwa na starting point yake na ending point yake
Mwisho ninaozungumzia hapa n mwisho wa miisho yoye
Yaani n muda ambapo ulimwengu wote na shughuli zake utafikia kikomo!
Nataka uone namna shetani anatumia maonyo hayo hayo ambayo Mungu ameachilia juu ya waamini kuwafanya wasione uhalisia wa kile Mungu anataka waone
Ngoja nkufikirishe kdgo
Unayaamini maandiko kwa kiwango gani??
Soma na Mimi mahala hapa alafu unjibu kwa kiwango gan unaamini maandiko na kile unachokisikia kwa watu
π Matayo:6.33
Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.
Nadhan wengi tumewah soma maneno haya
Nimewahi sikia watu wanasema ukijikuta hautafuti connections unategemea tu imani huna akili lkn maandiko yananiambia hivi utafute kwanza ufalme na haki yake
Nsiende mbali sana
Ngoja tuanze kutazama Siri zilizopo hapa kwenye kitabu cha Petro
Jambo la kwanza ninaloliona hapa biblia inakubali kabisa kwamba mwisho upo Mimi sijui Kama wewe unaamini au haumini
Lakin maadamu tu maandiko yamesema hvyo mm nalipokea na kukubaliana nalo bila Shaka hata kidgo
Na anasema very soon n karbu mno
Kama wakati anaandika miaka efu2 ilopita alisema n soon how about today?
Sikia Jambo lingine ninaloliona hapa ni hili iweni na akili(watchful) mkeshe *KATIKA* sala
Maana yake n kwamba n majira ambayo kaama tutaenda tu katika sala au kuomba alafu hatuna akili(taarifa sahihi za NENO LA MUNGU) kuna mahala tutakwama
Maana yake pia n kwamba kadiri tunavyozidi kusogelea miisho ndvyo tunayahitaji maombi na taarifa za neno kuliko kipindi kingine chochote
Shetani kwa kulijua hili angalia alichokifanya kwa wana wa Mungu
Alipogundua kanisa linatakiwa lishughulike na ufalme wa Mungu kwanza akapachika mahubir ya mafanikio kanisani kias ambacho Wana wengi wa Mungu wanajikuta wanashughulika na mafanikio ya kiuchumi kuliko roho zao
Kuna mtu hajanielewa sipingani na maandiko yasemayo tunatakiwa kuwa matajiri rahasha.........
Nielewe
Namaaanisha protocol inatakiwa kuzingatiwa
Sipo hapa kuchambua dini au kanisa nakupa neno la biblia
Angalia leo hii semina unazoenda zinakuunganisha na Mungu kuandaa moyo wako kwa ajili ya hukumu?
Au zinakuandaa kukufanya kuwa tajiri lkn hawez kuongea na Mungu Wala hana mahusiano binafsi na Mungu?
kwanini unabii mwingi now days iwe ninaona gari linakuja kwako naona unajenga nyumba
Cjakataa kuwa hayo Mungu anaweza kufanya
Lakini sitaki kukubaliana nawewe kwamba Mungu atakuletea unabii wa kununua gari na anajua hata ukifa hapo huendi mbinguni
Unasema kwann
Angalia maandiko yasemavyo
Kuokoka kwa mwenye dhambi mmoja ni Furaha kubwa mbinguni na jeshi la malaika waliopo kule
Umewah soma mahali maandiko yanasema kununua gar au kujenga kwa mtu mmoja n furaha kubwa mbinguni nionyeshe iyo sehemu
Nataka unielewe vzur
Ipo hvi mafanikio ya kiuchumi nk nk yanatakiwa kuwa matokeo ya mahusiano yako na Mungu
Mpenzi ufanikiwe Kama roho yako ifanikiwavyo.
Angalia kuna watu wanajua ahadi za kufanikishwa tu akn hana uhakika kabisa Kama Yesu akishuka hapa Leo atakuwa kwenye kundi lipi
*Are you prepared?*
*Neno linasema utafuteni kwanza!
Kwanza!
```Una uhakika Yesu ni Bwana na Mwokozi wa maisha yako?```
```Unao uhakika na kesho yako ukifa leo wapi utaenda?```
Anasema iweni na akili mkeshe
Na si kukesha tu lakni katika sala
You pray while watching through the revelation of truth
_Akili_
_Kukesha_
_Kuomba_
Soma na Mimi maandiko hayaππΏππΏ
π Matayo:15.8
Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami .
Matayo:15.9
Nao waniabudu bure,
Now days watu wanaenda kanisani sio wakasikie Mungu anasema nini juu ya roho zao wanataka kutabiriwa lini atajenga Lin ataoa we need to go back to Anguish of God
Anasema amesikia myasemayo kwa midomo, kuimba kwenu amesikia na hana tatzo navyo shida ipo kwenye eneo la moyo kwa sababu mioyo iko mbali naye
Yaani wayasemayo na yale yameujaza moyo n vitu viwili tofauti
Yaani n waamin kwa kuonekana kwao but infact mioyo yao ipo mahali kwngne
Kuna kitu kimekaa kwenye nafas aliyotakiwa kukaa Mungu
Are you prepared?
Haujiulizi n maeneo machache Sana leo hii wamekaza kufundsha watu watafute mahusiano binafsi na Mungu?
Now days kuna mahala haina haja ya wewe kuomba kwa sababu mtumishi ataomba aje akupe unabii imetoka ?
Ukiona umekaa mahali haufundshwi kuwa na mahusiano binafsi ya Mungu mahala hapo hapakufai hapakuandai na mwisho wa miisho
Hembu tufike mahala tuanze kujua kile Mungu anataka tukiishi
Moyo wako umeuelekeza wapi?
Una uhakika Yesu ana nafasi ya kwanza?
Are you sure?
Shetan alipojua unahitaji akili ya maandiko maarifa ya neno ili upate akili za kila Aina za kichwani na moyoni akakufanya uamini haujitaji kusoma neno unahitaji unabii tu na kuombea ili utoke hapo kwenda hatua ingine
My friend tutakupoteza
Anasema iweni na akili!
Iweni makini iweni waangalifu
Kwa tafsir hiyo kuna mahusiano makubwa Sana kati ya mwisho na akili yako
Unasema kivipi angalia maandiko haya!
Matayo:24.38
Kwa kuwa kama vile siku zile zilizokuwa kabla ya Gharika watu walivyokuwa wakila, na kunywa, wakioa na kuolewa, hata siku ile aliyoingia Nuhu katika safina,
Matayo:24.39
wasitambue, hata Gharika ikaja, ikawachukua wote, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.
Ukiyasoma vzuri maandiko haya utagundua kwamba watu wa enzi za Nuhu walikuwa wanaendelea na maisha ya kawaida ya kila siku
Kiasi ambacho kwa akili ya kawaida mtu hawezi kugundua Kama kuna jambo linakuja
Akili zimelala
Anaposema iweni na akili anajua kabisa ya kwamba kuna hatari ya kupumbazwa na kawaida ya dunia hii ukaona Kama hakuna kinacho endelea lkn infact muda upo mwishon
Sasa ili uweze kusoma majira na nyakati hizo unahitaji akili ya ziada ambayo utaipata kwa neno la ufunuo wa Mungu juu yako!
Amka amka
Naomba kwa leo tuishie hapa kipindi kijacho nitaanza kukuonesha mahusino ya hivyo vitu vitatu na mwisho wa miisho*
```Akili
Kukesha
Kuomba```
No comments:
Post a Comment