Popular Posts

Friday, May 15, 2020

MUNGU ANATAFUTA MTU WA KUMFUNUA DUNIAN

Bwana Yesu asifiwe Sana mtu wa Mungu  
Karibu tena tujifunze neno la Mungu

Ngoja nkutazamishe jambo hapa kabla cjaanza kuelekeza somo letu
Kwa wale ambao wanaifahamu Unaweza ukanielewa kwa haraka lakini 

 Crude oil 
Is complex mixture of hydrocarbons

Sasa ikiwa katika complex form huwa haina msaada lakini ili tuweze kupata faida ndani mwake lazima tuipitishe kwenye refining system ili tuweze kupata attributes tofauti tofaut Kama petrol , disel nk nk

Vivyo hvyo Mungu amejiweka katika mfumo ambao n very complex tunaitambua Kama (Holy spirit)

```Sasa Roho Mtakatifu yupo kwenye mfumo ambao n very complex lakin ili watu wa kawaida ya duniani wamuone katika uhalisia wake lazima kuwe na mchakato Fulani ndani yako ambao utamsaidia kujifunua kwao!!!```

Moja ya vitu ambavyo utakuja kugundua Ni kwamba Mungu huwa hafanyi Jambo lolote duniani bila ya kumpata mtu Kati wa kumuunganisha na mifumo ya huku ulimwenguni!!!

Nilifikir kwa kina
Alipokuwa amechukizwa na maovu ya watu wa kizaz Cha Nuhu hakutoa adhabu Moja kwa moja alimtumia Nuhu!!!
Alipokuwa anahukumu maovu ya kizazi Cha Sodoma na gomora alimtumia Luthu na Ibrahim!!!

Kwa mawazo yangu ya haraka haraka ilinipa ugumu kukubaliana na hali hiii yeye Kama Mungu muweza wa yote kwann asiwapige moja kwa moja kwa uweza wake

Si hivyo tuy wakati anataka kuwatoa wanna wa Israel kule misri hakuenda yeye Kama Yeye lakini sisi tunajua kabisa ya kwamba Ni Mungu ndye aliwaokoa!!!

Narudia Mungu anatafuta mtu wa kuelezea uhalisia wake katika Angle tofauti hapa duniani!!!

Child of God nielewe vzuri Mungu anataman sana tuone uhalisia wa uweza wake katika maisha yetu ya Kila siku!!!
Warumi:8.19

Kwa maana  viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu

```Uwe na uhakika kufunuliwa kwa wanna wa Mungu sio swala dogo kwa sababu kufunuliwa anakozungumzia Ni kule kuExpress a certain dimension of God```

Maana yangu n kwamba Kuna kitu Kinatakiwa kitokee kwenye maisha yako ya Kila siku ambacho sis tukikiona tumuona Mungu ndani ya maisha yako

Naomba tusome kitabu Cha matendo 1;8

Watu wengi huwa wanalielewa hili andiko katika Kona ya nguvu za kufanya miujiza na kutoa mapepo tuuy!!!

Lakin kwa kweli Nguvu hi ya kiungu ipo katika Kona nyingi Sana
Ndo maana nimekwambia Holy Spirit is in a very complex form!!!

Kwa mfano ngoja nkutazamishe maandiko machache
Luka:16.20
Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda vingi, 
Luka:16.21
naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri; hata mbwa wakaja wakamramba vidonda vyake. 
Luka:16.22
Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.

Ukisoma kwa makini habari hizi utagundua Kwamba Lazaro alikuwa hana utajr wa Mali ila alikuwa na utajiri wa upako au kwa lugha nyepesi alikuwa mtu wa kiroho usivyoweza kudhani na ndiyo maana Utaona kwamba the moment amekufa yupo kifuani pa Ibrahim ikiwa na maana kwamba maisha yake yote huyu jamaa aliiish kwa iman ya kufika mbinguni!!!

Na Utaona kabisa role model wake alikuwa Ibrahim yaan alikuwa anaishi maisha ya imani Kia's ambacho alifikia level za kuwa na iman inayofanana na ya Ibrahim
Ooh nataman uone hili jambo
Angalia Jambo lingine

Luka:4.14
Yesu akarudi kwa nguvu za Roho akenda Galilaya; habari zake zikaenea katika nchi zote za kandokando

Hapa ni Yesu akiwa ametoka kwenye mfungo wa siku arobaini mfululizo bila kula chochote!!!

Kwa hali ya kawaida alikuwa kaishiwa Nguvu mwilini lakin kwa Nguvu ya Roho Mtakatifu alikuja na uzima!!!

Kwa hyo hiii Nguvu ipo kwenye dimensions tofauti tofauti!

Kumbukumbu La Torati:8.18
Bali utamkumbuka Bwana, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.

Ni Nguvu ile Ile ya matendo 1:8 hapa ikiwa inaelezea dimensions ya kupata itajiri!!!
Kwa sababu bado Ni kwa ajili ya ufalme!!!

Nataman upate picha halisi hapa
Sasa Kuna category tofauti tofaut za kuelezea uhalisia wa Mungu(kumfunua Mungu) duniani


Your life can be a blessing and a dimension God's ability on Earth!!!

Jambo la kwanza unalo hitaji Ni Power of the Holy spirit
ngoja nkuoneshe andiko kidogo

Matendo ya Mitume:10.38
habari za Yesu wa Nazareti, jinsi Mungu alivyomtia mafuta kwa Roho Mtakatifu na nguvu naye akazunguka huko na huko, akitenda kazi njema na kuponya wote walioonewa na Ibilisi; kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.

Hapa nataka uone Mambo mawili ya muhimu
Jambo la Kwanza kumtia mafuta(to anoint) by the holy spirit

Jambo la pili Ni kumtia mafuta(to anoint) kwa Nguvu by power (dunamiss    power)

Ukitazama kwa makini Utaona Kuna Mambo mawili yanahitaji kutokea ili mtu aanze Kimtambulisha Mungu mahali kwa viwango ambavyo anakuwa Ni halisi kwa Kila anayekutazama wewe

You need be anointed by the person of the Holy spirit (his personality to be yours)

To anoint is to be given an authorization over something

Tunaposema Mungu amekuAoint it is something like umepewa nature ya namna ya kiungu ambayo kwa Namna ya kawaida usingeweza kuwa nayo
Ngoja nkuelezee kidgo hapa

Isaya:61.1
Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu;  kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao

Ukisoma andiko hili Utaona kabisa huyu jamaa alikuwa n mtumishi wa Jehovah lakini kabla Roho wa Bwana( Roho Mtakatifu) hajakaa juu Yake hajawa sehemu ya utumishi wake Kuna Mambo alikuwa hana uwezo wa kuyafanya lakini alikuwa mtumishi wa Mungu!!!

Lakn baada ya mchakato wa kuwa anointed kinachotokea anaanza kuOperate supernatural things in a natural rhealm

Anasema amenipaka mafuta(he has anointed me) to do something!!!

Kwa lugha hiii utagundua Kwamba kuwa anointed n kupewa uwezo ambao umebeba uungu na Umungu ndani mwake

Turudi kwenye point yetu ya Kwanza anaposema kupakwa mafuta kwa Roho Mtakatifu na kwa Nguvu

1. Roho Mtakatifu nilianza kukueleza he is a very complex personality
Kwa hiyo anapokuwa introduced ndani yako yaanzi tu kuyaendesha maisha yako
He is a very gentle personality as well
Anahitaji ruhusa yako kuyaendesha na kuyaongoza maisha yako

Sasa anaweza akawa ndan yako na bado ukashindwa kumfunua Mungu mahali ulipo kwa sababu Kuna mchakato haujachukua nafasi ndani mwako

Ngoja nkueleze Jambo hapa
Roho Mtakatifu anapokuja ndani mwako kiu Yake kubwa Ni kukufanya wewe kuwa wake kwa maana ya Kila kitu kuhusu wewe kuwa under his authority lakin kwa ruhusa yako

Anataka akupitishe kwenye mambo kadha kadhaa ili Sasa aanze kukutumia Kimtambulisha Mungu kwa watu waliopo kwenye hilo eneo!!!

Eneo la Kwanza analoanza kushughulikia n utu wako wa asili au tabia zako kwa lugha nyepesi

Kwa sababu tuliona mtu wa asili hawezi kupokea Mambo ya Roho wa Mungu
Ndyo maana kuamka usiku kuomba sio swala la kimwili you need to be empowered by him

Swala la kutokasirika ovyo ovyo swala la kutojadili watu badala ya Yesu madhabahuni n swala la kiroho Sasa Kama Ndani yako haja shughulikia ipasavyo huwezi Kimtambulisha Mungu !!!!

Ngoja nkupe mfano
Yohana mbatizaji maandiko ynatuambia alijazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama Yake

Ila kilichonipa shida kuelewa n kwann hakuanza moja kwa moja kumfunua Mungu kwenye eneo alilopewa Kimtambulisha Mungu!!!?

Nkaja kuona huyu jamaa alikaa jangwani(nyikani) kwa muda mrefu Sana na maandiko yanatuambia alikuwa akila asali na ngize n mazingra Magumu Sana haya!!!

Na Nina uhakika Roho Mtakatifu alimpeleka kwenye mifungo na kuomba kwingi mno katika hicho kipindi
Kwann kwa sababu moja ya Mambo Roho Mtakatifu atafanya n kuhakikisha anaua utu wako wa asili(your flesh) kias ambacho Roho yako inakuwa dominant kwenye Kila kitu kuhusu wewe
Na Utaona Yohana alikuja Yordan Biblia inasema nji nzima na zote zilizokuwa kando kando walimjia kumsiliza
This is a result of being anointed!!!

Kuna watu wanashindwa kutofautisha Kati ya kuwa imparted na kuwa anointed!!!
Sikilza huyu jamaa alikuwa kashaa zalisha upako Kia's Cha kuhudumia mataifa your hayo!!!

Hapa uwe na uhakika alikuwa hajitazami yeye alikuwa n krsto ndani mwake(Roho ndani mwake)
God is all he lived for!!!!

Nadhani umenielewa kwamba kuwa na Roho Mtakatifu Ni Jambo moja kutembea katika utu wake au kutembea naye n Jambo lingine you need fasting and prayers non ceasing ones
Mungu anataman kuona unamtafuta Kias ambacho he will make himself known to you!!!

Jambo la pili to anoint by power Ni matokeo ya wewe kutembea na Roho Mtakatifu mpaka anakuwa yeye ndiye Nguvu yako ndye maarifa yako ndye Kila kitu chako he becomes the all that you have!!!!

Matendo 1;8

Monday, May 11, 2020

JIZOEZE KUTAFSIRI MAMBO KIROHO ILI UTEMBEE KWENYE UKUU WA KIUNGU


Kwanini ninasema hivi
Kwa sababu nimekuja kugundua kwamba Kuna Mambo mengi Sana amabyo Mungu hutaman yatufukie kwa wakati lakini huwa inakuwa vigumu sisi kuchukulia uzito kwa sababu tunatembea Sana na mitazamo ya kibanadamu kuliko tunavyotafsir kiroho

Kuna Mambo ukiyatazama kwa namna ya kawaida huwezi kuona mpango madhubuti wa Mungu ndani yake

Umewahi kujiuliza kwann Paulo alikaza Sana kuombea kanisa la Efeso juu wao kuwa na namna ya kiungu ya kutazama mambo!!!

Waefeso:1.18
macho ya mioyo yenu yatiwe nuru mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo;

Ukitazama kwa makini Utaona kabisa msisitzo wa Paulo upo kwenye uwezo wa mioyo yao kuona

Kumbuka kuona kwamba moyo Ni pamoja na Namna mtu anavyo uafasr Mambo anayokutana nayo Kila siku
Anasema macho yatiwe nuru(yapewe uwezo/power) to see in Godly way the things of our everyday lives

Kwann macho yatiwe nuru(ya kiungu)

Tazama maneno haya
1 Wakorinto:2.14

Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni

Maana yake nn
Tafsr Yake n kwamba kuna vitu vingi Sana Mungu huwa anavipitisha kwenye maisha Yetu ya Kila siku na tunayaona kwa jicho la asili(kibinadamu) na kwa sababu hiyo tunakosa uwezo wa kuona kitu au faida za kiroho(kiungu) zilizomo ndani mwake

Nataman nikitazamishe Mambo kadhaa kwenye maandiko uyaona kwa undani

2 Wakorinto:4.4
ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu.

Ukitazama tofauti ya mtu mwamini na mtu asiyemwamini n utendaj Kaz wao wa utu wa ndanj
Kuna mmoja ana Fikra zinazoona Kiroho Kuna mwingine ana upofu hawez kuona Kiroho

Maana yake n kwamba katika uhalisia wa kiungu haoni chochote anaona uhalisia wa Jambo hilo kimwili ambalo kwa kweli Lina uhalisia mkubwa Zaid Kiroho kuliko mwilin anakoona yeye

Ngoja nkupe mfano
Bila Shaka umewah kusoma habr za kuzaliwa kwake mwokozi(Yesu) katika kitabu Cha Mathayo

Ngoja tutazame kwa pamoja
Utaona kabisa Yusufu na marina walikuwa kwenye hatua ya uchumba
Lakin Cha ajabu Mariam alikuwa tyr ana mimba ambayo kimsingi sisi tunajua kabisa n matokeo ya Roho mtakatifu kuja kutimiza kusudi maalumu

Na Jambo lilinishangaza Ni kuona Namna Yusufu alivyo fanya maamuzi juu ya mimba aliyoiona kwa mchumba wake na kwa kweli haikuwa ya kwake na hakujua n ya nan
Maandiko yanasema akaazimu moyoni mwake  kumwacha kwa Siri

Kwann kwa sababu alikuwa mtu mwenye haki(mtu wa kiroho) Kia's ambacho pamoja na kwamba mchumba wake ameamua kumasaliti lakini hakutaka kufanya liwe Jambo la kumuabisha

Usifikir ulikuwa n wakati mwepes kwa Yusufu uwe na uhakika alikuwa na mawazo na wakati mgumu Sana lakini alifanya maamuzi kiroho
No wonder Mungu aliamua kuptisha kusudi la kuukomboa ulimwengu mikononi mwa Yusufu

Jambo lingine utakaloliona Ni kwamba Yusufu alianza alifanya uamuzi wa kufikiri Nina uhakika kabisa aliingia kuomba hekima mbele za Mungu kujua Nini afanye juu ya usaliti huu wa mchumba wake!!!!

Hili linanipa kabisa kuona Namna Yusufu alivyokuwa anafasir Mambo kiroho na kumsaidia kutembea kwenye mapenzi ya Mungu!!!

Matayo:1.20
Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

Utagundua Kwamba kufikiri kwake hakukuwa kufikir kwa kawaida alikuwa anafikri huku anaomba maongozi ya Roho Mtakatifu juu ya Nini afanye juu ya Mariam
Kwann ninasema hivi kwa Sababu Malaika alipomjia Ndotoni akamwambia asihofu kumchukua 

Hili linanipa uhakika ya kwambaa alikuwa anajiuliza Kama amchukue na mimba asiyojua n ya Nani au asimchukue!!!!!

Malaika aalileta majibu ya maombi hayo

Sasa Jambo lingine utakaloliona hapa Ni mfumo wa  ujio wa ujumbe serious Kia's hiki Kuja kwa Yusufu
Kumbuka majibu ya maombi hayo yalikuwa n majibu yanayobeba wokovu wa ulimwengu wote

Kumbuka hapa n swala la kuzaliwa kwa Yesu mwokozi wa ulimwengu

Kilichonipa shida kuelewa n kuona Majibu ya Maombi hayo yanakuja kupitia ndoto

Nilitegemea Mungu azungumze naye kwa malaika live au yeye mwenyewe lakin alikuja Ndotoni
Nikafikir ndoto ambazo zimekuwa zikipita ndani mwangu na uzito ambao huwa ninazipa nikagundua Kuna Mambo mengi Sana ambayo sikuwa serious nayo

Kumbuka utii wa Yusufu juu ya ndoto uliokoa maisha ulimwengu mzima
Kuzaliwa kwa Yesu
Tazama namm hapa

Ayubu:33.14
Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali.
 
Ayubu:33.15
Katika ndoto katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani;

Ukisoma hapa utagundua kabisa Mungu huwa anasema na mioyo ya watu kupitia ndoto ila Ni wachache Sana wanaofasr kiroho ndoto wanazoziota!!!!

Nlipogundua hili binafsi nilianza kuandika Kila ndoto ninayoota na kuanza kutafuta maana yake na ujumbe uliomo ndani mwake

Nimeona matunda yake

Wewe unapoota huwa unalichuliaje swala la ndoto ???

Pengine ungetii ndoto uliyoota ungekuwa umepiga hatua kubwa Sana Katika maisha yako kiroho, kiuchumi nk nk

Jizoeze kufasir Mambo kiroho kwa sababu kuna Siri kubwa ndani mwake
MUNGU AKUBARIKI